الموضوع: Maana ya Adhana na Ikama
عرض مشاركة واحدة
  مشاركة رقم : 1  
قديم 02-16-2020
غرير غازي


رقم العضوية : 606
تاريخ التسجيل : Jan 2020
الدولة : مصر
المشاركات : 22
بمعدل : 0.01 يوميا
معدل تقييم المستوى : 0
المستوى : غرير غازي نشيط

غرير غازي غير متواجد حالياً عرض البوم صور غرير غازي



المنتدى : English Forum
افتراضي Maana ya Adhana na Ikama

[INDENT][INDENT]Ni kujulisha kuingia wakati wa Swala kwa kuleta maneno maalumu ya dhikiri.

Kukimu
Ni kujulisha kuanza kuswaliwa kwa kuleta maneno maalumu ya dhikiri.

Hukumu ya kuadhini na kukimu
1. Katika Swalah za jamaa:
Ni faradhi ya kutosheleza, kwa Swalah tano za faradhi peke yake, safarini na mjini, kwa kuwa hizo mbili ni miongoni mwa alama za Uislamu za waziwazi, hivyo basi haifai kuziacha. Amesema Mtume ﷺ: (Ufikapo Wakati wa Swala, basi awaadhinie mmoja wenu, kisha awaswalishe mkubwa wenu) [ Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

2. Katika Swalah ya anayeswali peke yake:
Ni sunna. Amepokewa ‹Uqbah bin ‹Amir akisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema: (Anamuonea ajabu Mola wako mchunga mbuzi aliye juu ya kilele [ Shadhiyyah: Ni kipande kilichoinuka kilichoko kwenye kilele cha jabali.] cha jabali, anayeadhini kwa Swala kisha akaswali, hapo aseme Mwenyezi Mungu Aliyetukuka: “Mwangalieni mja wangu huyu, anaadhini kisha anakimu Swala, ananiogopa! Nishamsamehe mja wangu na nitamuingiza Peponi”) [ Imepokewa na Annasai.].

Hikma ya kuadhini

1. Kujulisha kuwa wakati wa swala umeingia.

2. Kuhimiza juu ya Swalah ya jamaa.

توقيع غرير غازي

[سجل معنا ليظهر الرابط. ]


رد مع اقتباس